SEHEMU YA KWANZA
Nakumbuka ulikuwa ni mwaka 2010, nilipata bahati ya kufanya kazi za ndani katika nyumba moja iliyokuwepo maeneo ya Kijitonyama. Ilikuwa ni familia ya Mzee Gidion pamoja na mke wake ambapo katika maisha yao walifanikiwa kupata watoto wawili, mtoto wa kwanza alikuwa ni wa kiume aliyejulikana kwa jina la Daniel na mwingine wa mwisho alikuwa ni wa kike aliyejulikana kwa jina la Naomi.
Mzee Gidion alikuwa akimiliki kampuni moja hapa mjini iliyomuingizia kiasi kikubwa cha pesa, aliishi maisha mazuri yeye pamoja na familia yake.
Baada ya kupita miezi mitatu tangu nilipoanza kufanya kazi za ndani katika nyumba hiyo Mzee Gidion alianza kunitamani, alichokuwa akikihitaji ni penzi langu tu, aliahidi kunifanyia mambo mengi sana katika maisha yangu endapo kama ningekubali ombi lake la kulala naye kitanda kimoja.
Kiukweli lilikuwa ni jambo gumu mno hasa ukizingatia mke wake ndiye aliyenileta katika nyumba hiyo kwa lengo la kufanya kazi, sikuwa tayari kumkubalia ombi lake lakini kutokana na tamaa za pesa zilizoniingia nikajikuta nikimkubalia na kuanzisha mahusiano naye ya kimapenzi.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kushiriki mapenzi tangu nizaliwe, Mzee Gidion ndiye alikuwa mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu, alionekana kufurahishwa sana na kitendo hicho, kwanza hakutegemea kama angeweza kunikuta na usichana wangu mpaka kufikia umri wa miaka ishirini niliyokuwa nayo, hilo lilizidi kumfurahisha mno.
Niliendelea kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Mzee huyo ambaye aliniambia nilitakiwa kufanya siri, hakutaka mke wake afahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Alinitahadharisha niwe makini kwani kama mke wake angeweza kufahamu mahusiano yetu ningejiingiza katika matatizo makubwa.
Hilo halikuwa tatizo, niliendelea kuwa katika mahusiano na Mzee Gidion huku penzi lake likizidi kuniteka. Ukumbuke kuwa Mzee Gidion ndiye alikuwa mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu, alikuwa amenifungulia dunia mpya ya mapenzi, hapo kabla nilikuwa ni mtu wa kuyasikia mapenzi jinsi ambavyo watu walivyokuwa wakiyasifia pamoja na utamu wake, sikuwa nikifahamu lolote kuhusu mhemko na raha ambazo mtu alikuwa akizipata wakati akifanya mapenzi.
Tangu nilipofanikiwa kufanya mapenzi kwa mara ya kwanza na Mzee Gidion nilijihisi kuwa kiumbe kipya, nilijiona kukamilika kuwa msichana.
Kipindi hicho Mzee Gidion alianza kunijali, alikuwa akinipa kiasi cha pesa chochote nilichokuwa nikikihitaji.
"Msichana mrembo kama wewe unatakiwa uwe na simu kali, upendeze yaani ubadilike, uishi kimjinimjini, nitahakikisha nayabadilisha maisha yako Mwajuma," aliniambia Mzee Gidion.
"Nitashukuru Baba," nilimwambia.
"Usiniite Baba, sifananii kuwa Baba yako mzazi hata wa kuchorwa, niite mpenzi au Gidion tu inatosha," aliniambia.
Kwa kumtazama Mzee Gidion alionekana kuwa Baba yangu kabisa, alikuwa ni Mzee wa makamo ambaye alifanikiwa kuwa na watoto wawili. Kipindi hicho Daniel ambaye ndiye mtoto wake wa kwanza alikuwa akisoma chuo kikuu cha Daresalaam, alikuwa akisomea sheria, ulikuwa ni mwaka wake wa pili.
Kwa upande wa Naomi alikuwa kidato cha tatu, alikuwa akisoma Morogoro katika shule moja ya bweni, maisha yake yote yalihamia huko mpaka wakati wa likizo ulipofika ndipo ambapo aliweza kurudi nyumbani.
Unaweza ukaona jinsi ambavyo maisha yalivyokuwa katika nyumba hiyo, kila mtu alionekana kuwa bize na mambo yake, kuanzia Mama, Baba na watoto, muda mwingi nilibaki peke yangu nyumbani.
Mzee Gidion aliitumia nafasi hiyo kuwa fursa ya kuwa karibu na mimi. Aliamua kuninunulia simu kwa lengo la mawasiliano, alihitaji kuwasiliana na mimi zaidi na zaidi.
Siku ziliendelea kukatika huku penzi kati yangu na Mzee Gidion likizidi kupamba moto. Alipanga kuninunulia nyumba pamoja na gari la kifahari kwa dhumuni la kunihamisha nyumbani hapo, hakutaka kuona mapenzi yetu yakiendelea kuwa siri, alinogewa na utamu wa penzi langu.
Nilijisikia furaha sana kusikia hivyo, niliamini huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kusahau umasikini niliyotoka nao nyumbani kwetu Mtwara.
Kila kitu kilichokuwa kikiendelea kiliniweka katika wakati wa furaha sana, nilizidi kumpenda Mzee Gidion, nilisahau kama alikuwa ni mume wa mwanamke aliyenitoa kijijini na kunileta mjini kwa lengo la kufanya kazi, ahadi nilizowaahidi wazazi wangu pamoja na kiapo nilichokiapa mbele yao kwa wakati huo nilikuwa nipo kinyume kabisa.
INAENDELEAAA......
SEHEMU YA PILI
Katika kipindi hicho ambapo nilikuwa katika mapenzi na Mzee Gidion, Daniel mtoto wa Mzee huyo na yeye alianza kunitamani, sijui nilimvutia na nini ila nilishangaa akinitongoza, alionekana kunihitaji kupita maelezo.
"Daniel embu acha kunitania bhana," nilimwambia huku nikionekana kutomuamini kabisa.
"Sikutanii Mwajuma kweli nakupenda, nahitaji kuwa na wewe," aliniambia Daniel.
"Umenipendea nini sasa?" nilimuuliza.
"Vingi tu vingine siwezi kukuambia," alinijibu.
Unajua kwanini sikuweza kumuamini Daniel? Kwanza alikuwa ni mtoto aliyetokea katika familia ya kitajiri, alikuwa ni msomi ukiachana na mimi ambaye nilifeli kidato cha nne, pili alikuwa ni handsome, alivutia mno, kwa kumtazama ilikuwa ni vigumu kuamini mvulana kama yeye kukosa msichana.
Alinisumbua sana, kila siku ombi lake lilikuwa ni moja, kuna kipindi nilimuonea huruma alipoingia chumbani kwangu kisha akawa ananibembeleza nimkubalie. Haikuwa rahisi kumkubalia kwani tayari nilikuwa katika mapenzi mazito na Baba yake na tulikuwa kwenye mipango mingi, nilikuwa nikisubiria itimie.
"Hapana Daniel siwezi kukubali hilo litokee wewe ni kama kaka yangu," nilimwambia Daniel.
"Mwajuma nakupenda, macho yangu yamekutazama wewe, una kila sababu za kuwa na mimi, umeuteka moyo wangu wa mapenzi tafadhali naomba usiuumize nitakufa," aliniambia Daniel huku machozi yakimlengalenga.
Nilishindwa kuvumilia kumuona Daniel akiendelea kuteseka kwa ajili yangu, nilimuonea huruma sana, mwisho wa siku nikajikuta nikishawishika na kumkubalia tukawa wapenzi.
Daniel alifurahi sana, hakuamini kama alifanikiwa kunipata huku nyuma ya pazia hakujua nini kilichokuwa kikiendelea kati yangu na Baba yake.
Kitendo cha kumchanganya Baba na mtoto kimapenzi hakika kilikuwa ni hatarishi sana, sikutaka kumwambia lolote Daniel, nilihofia mambo mengi mabaya ambayo yangeweza kunitokea.
Nilizidi kufaidi utamu wa penzi la Baba na mtoto huku kila mmoja kwa nafasi yake akikiri kunipenda kupita kawaida.
Siku ziliendelea kukatika, Mzee Gidion alianza kuingiwa na wasiwasi juu yangu, alihisi kuna mchezo mchafu ambao nilikuwa nikimchezea, hakutaka kuamini jambo hilo hata mara moja, alianza kufanya uchunguzi wake na mwisho wa siku akafanikiwa kugundua kuwa nilikuwa nikitembea na mtoto wake. Hilo lilimuumiza sana, alinilaumu mno. Naweza kusema siku hiyo ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwanza kumuona mwanaume mtu mzima kama Mzee Gidion akilia mbele yangu huku sababu ikiwa ni mapenzi, hakutaka kuamini kama yeye pamoja na mtoto wake walishiriki mapenzi na mimi.
Mzee Gidion alipagawa, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea, moyo wake ulimuuma mno, aliponitazama alionekana kuwa mwenye hasira, machozi yalikuwa yakimdondoka kwa wakati huo.
Nilishindwa kuamua la kufanya kwani mpaka kufikia muda huo nilikuwa tayari nimeshafanya makosa. Kwanza nilikuwa nikitembea na mume wa mtu kwa kujua, pili niliwachanganya kimapenzi baba na mtoto. Haya yalikuwa ni makosa ambayo kiukweli sikuwahi kukaa na kuwaza kwamba kuna siku yangeweza kunigharimu maisha yangu.
Nilishindwa kuvumilia kumuona Mzee Gidion akiendelea kulia mbele yangu kama mtoto mdogo, ilibidi nimsimulie kila kitu kilichotokea kwa Daniel mpaka nikajikuta nikimkubalia na kuwa wapenzi, sikuacha kumuomba msamaha kwa kosa nililokuwa nimelifanya, nilikiri kukosea na kumuahidi kutorudia tena makosa.
Baada ya kumueleza hayo pamoja na kumuomba samahani Mzee Gidion hakutaka kunielewa kabisa, alinichukia, alinifananisha na kahaba ambaye nilikuja kwenye familia yake kwa lengo la kutembea na ukoo mzima.
Hilo lilizidi kuniumiza mno, kitendo cha kuniita kahaba ambaye nilikuja kwenye familia yake kwa lengo la kutembea na ukoo mzima hakika kiliniumiza sana, moyo wangu ulikuwa kwenye maumivu makali mno.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuishi maisha ya visasi kila siku, Mzee Gidion alikuwa ni mtu wa kunitishia maisha, alinikosesha amani ya moyo niliyoishi nayo kwa muda mrefu, sikuwa huru tena, muda wote nilikuwa nikimfikiria pamoja na vitisho alivyokuwa akinipa.
Kuna kipindi nilitamani kumueleza mke wake ukweli wote wa kile kilichokuwa kikiendelea kati yangu na mume wake lakini unafikiri ningeanzia wapi? Ningeupatia wapi ujasiri huo wa kumueleza kila kitu na wakati hapohapo tayari nilishamkosea kwa kitendo cha kutembea na mume wake.
Hiyo iliendelea kubaki siri ya moyo wangu, siri iliyokuwa ikinitesa mno. Mzee Gidion hakuacha kushiriki kufanya mapenzi na mimi, aliendelea kunitumia kimwili lakini safari hii haikuwa kama hapo awali, alibadilika na alikuwa akifanya mapenzi na mimi kama sehemu moja wapo ya starehe, yaani alinifanya kuwa kama kahaba ambaye alinitumia wakati alipohitaji kufanya mapenzi tu. Hilo liliniumiza sana, siwezi kusema ni maumivu kiasi gani niliyokuwa nayo katika moyo wangu lakini naweza kusema tamaa zangu za pesa ndizo zilizonipelekea nipitie katika wakati huu mgumu.
Daniel alikuwa ndiye mtu wa kwanza kuigundua tofauti yangu japo Mama yake alianza kuniuliza kuhusu mabadiliko yangu lakini nilimficha, sikutaka kumueleza ukweli.
"Niambie nini kinachokusumbua mpenzi, malaika, mke, malkia wa maisha yangu," aliniuliza Daniel.
"Hakuna kitu," nilimjibu.
ITAENDELEAAAA....
SEHEMU YA TATU
"Usiniambie hakuna kitu wakati nikikuangalia nakuona kabisa kuna kitu unanificha," aliniambia.
"Kweli hakuna kitu."
"Usinifiche tafadhali."
"Naogopa kukuambia Daniel."
"Unaogopa nini wewe niambie au mimba imengia?"
"Hapana bora ingekuwa mimba ningejua baba yake yupo."
"Ni nini sasa?"
"Ni kuhusu baba yako."
"Amefanyaje?" aliniuliza Daniel kisha nikaanza kumsimulia kila kitu. Nilipomaliza kumsimulia nikamuona akivuta pumzi ndefu na kuziachia kwa pupa, kama ilivyokuwa kwa Baba yake na yeye pia hakutaka kuamini, kitendo cha kuwachanganya kimapenzi na Baba yake kilimuumiza mno.
Nilishangazwa na maamuzi aliyoyachukua Daniel, hakutaka kuendelea kuushuhudia uchafu kama huo ukiendelea mbele yake, alichoamua kukifanya ni kuniambia kuwa siku hiyo ndiyo ulikuwa mwanzo na mwisho wa mapenzi yetu, hakutaka kusikia nikimuita mpenzi tena.
Niliumia sana baada ya Daniel kuchukua maamuzi hayo, mtu ambaye niliamini ndiye angeweza kuwa msaada wangu kwa wakati huo hakutaka kunisikia hata mara moja.
Maisha yalibadilika ndani ya nyumba, kila siku nilikuwa ni mtu wa kumuomba Mungu aninusuru na mabaya ambayo yangeweza kunitokea. Nilifahamu hapakuwa na amani tena, kuanzia Baba na Mtoto wote walikuwa na visasi juu yangu, hawakunitazama kwa macho ya wema tena, nilionekana kuwa mbaya tena adui mkubwa ambaye walitakiwa kuniepuka.
Vitisho havikuishia hapo, Mzee Gidion aliendelea kunitishia kuniua kila kukicha, wakati mwingine alikuwa akiniambia ni lazima niondoke katika nyumba yake nikiwa maiti ndani ya jeneza.
Wakati yote haya yakiendelea mke wake alikuwa hafahamu lolote, iliendelea kubaki siri katika moyo wangu mpaka pale nilipoanza kukosa uvumilivu, nilitishiwa sana, sikuwa na amani tena katika moyo wangu, uhuru wangu wote ulipotea, nilikuwa nikiishi maisha kama ya mfungwa aliyetoroka gerezani.
Wazo la kutoroka likanijia kichwani, nilichokuwa nikikiwaza kwa wakati huo ni kutoroka na kwenda mbali. Sikuwa mwenyeji wa jiji la Daresalaam, tangu nilipoweza kufika kwa mara ya kwanza maisha yangu yote yalikuwa ni ya kukaa ndani, labda siku moja moja za wikiendi niliweza kupata bahati ya kupelekwa katika fukwe za Coco ambapo hata njia ya kufikia huko nilikuwa siifahamu.
Nadhani unaweza ukaona ni kwa jinsi gani nilivyokuwa mgeni katika jiji hili. Wakati ambapo nilikuwa sifahamu mtaa hata mmoja tayari nilikuwa nimejiwa na wazo la kutoroka. Unafikiri nilifanikiwa katika mpango huu? Jibu ni hapana, niliendelea kujiuliza maswali ambayo yalizidi kuniumiza kichwa.
Inaendeleaaah
SEHEMU YA NNE
Ni katika kipindi hicho ambapo kumbukumbu za nyumbani kwetu zikaanza kunijia, nilipakumbuka mno, nilitamani kuambiwa kuwa nilitakiwa kurudi nyumbani kwetu lakini jambo hilo halikuweza kutokea hata mara moja.
SEHEMU YA TANO
Nilianza kuingiwa na wasiwasi baada ya kuwaona wakizidi kukazana kunifikia, moyo wangu ukalipuka paaa!! hofu ikanitawala, mapigo ya moyo wangu yakaanza kunienda kasi.
"Habari yako binti," alinisalimia mwanaume mmoja huku yule mwingine nikimuona akiangalia huku na kule, nilifahamu hawakuwa na nia nzuri na mimi. Hofu ikazidi kunitawala.
"Nzuri," nilijibu huku nikitetemeka.
"Mbona unaogopa usiogope sisi ni watu wazuri unaitwa nani?" aliniuliza yule mwanaume mwingine.
"Naitwa Mwajuma,"nilimjibu.
Walitazamana kisha wakapeana ishara fulani, sikujua walimaanisha nini ila nikashangaa wakinisogelea, ghafla! yule mwanaume wa kwanza akanirukia na kunikaba, nilishtukia nikipigwa na ubapa wa panga kwenye paja na kuambiwa nisipige kelele na endapo kama ningekiuka agizo hilo ningeweza kuuliwa, niliogopa mno, nilibaki nikiugulia maumivu ya ubapa wa panga pamoja na kabali niliyokuwa nimepigwa.
Yule mwanaume mwingine alianza kunisachi, akachukua simu, pesa pamoja na lile begi la nguo. Alipojiridhisha kuwa alifanikiwa kuchukua kila kitu changu alimpa ishara mwenzake na ndipo hapo alipoweza kuniachia.
"Sasa sikia wewe fala ukipiga kelele tunakuua, kaa kimya hivyohivyo," aliniambia kisha akanitukana tusi la nguoni.
Nikabaki kimya huku nikiendelea kuugulia maumivu niliyoyapata. Wale wanaume wakakimbia eneo hilo.
Wakati nikiendelea kuugulia maumivu huku nikiwa sijui nini nifanye mara akatokea mwanaume mmoja ambapo aliponiona alinifuata na kuniuliza nilikuwa na tatizo gani?
"Nimeibiwa kaka yangu, wameniibia," nilimwambia huku nikionekana kuchanganyikiwa.
"Embu subiri kwanza akina nani hao wamekuibia?" aliniuliza.
"Siwajui, siwajui kaka angu" nilimjibu huku nikianza kulia.
"Usilie sasa taratibu niambie kwanza unatokea wapi na unaitwa nani?"
"Naitwa Mwajuma nimetokea huko nilipokuwa nafanya kazi za ndani."
"Wapi?"
"Kijitonyama."
"Sasa huku umekuja kufanyaje?"
"Wapi?"
"Kwani unajua hapa upo wapi?"
"Hapana sijui kaka angu kwani hapa ni wapi?
" Tandale," alinijibu kisha akaanza kunionea huruma,
"Umesema umetokea Kijitonyama?'
" Ndiyo."
"Kwanini sasa wamekuruhusu kuja sehemu kama hii usiku?"
"Hapana nimefukuzwa," nilimjibu kisha akaonekana kunihurumia zaidi.
Mpaka kufikia muda huo nilikuwa bado sijalifahamu jina lake, alinitazama kama niliumia sana lakini hakukuwa na majeraha niliyoyapata zaidi ya kuugulia maumivu ya ndani kwa ndani. Hakutaka kuona nikiendelea kubaki eneo hilo kwani aliniambia mtaa huo palikuwa na vibaka wengi sana, hakuishia hapo alizidi kunipa sofa mbaya za mtaa huo hivyo kitendo cha mimi kuendelea kuwepo mahali hapo kingeweza kunihatarishia maisha yangu.
Baada ya kusikia kuwa nilifukuzwa na sikuwa na mahali pa kwenda usiku huo, alihitaji kunisaidia. Aliniambia alikuwa akiishi peke yake hivyo kama nisinge jali anichuke na kwenda naye kwake usiku huo.
ITAENDELEA
SEHEMU YA SITA
Kiukweli sikuweza kumkubalia kirahisi, nilihofia mambo mengi mabaya ambayo angeweza kunifanyia lakini baada ya kunohakikishia kuwa ningekuwa salama na kuniondoa hofu ilibidi nimkubalie. Akanichukua na kunipeleka mpaka kwake.
SEHEMU YA SABA
"Binti utajiingiza katika matatizo huyo unayeishi naye ni mume wa mtu," aliniambia Mama mmoja niliyemfahamu kwa jina la Mama Musa.
"Si kweli," nilimwambia huku nikiamini hakukuwa na ukweli wowote.
"Shauri yako binti unachokitafuta utakipata tu," aliniambia huku akionekana kunihurumia.
Bado sikutaka kuyaamini maneno yao, niliendelea kuwa katika mahusiano na Oscar. Miezi iliendelea kukatika hatimaye mwaka huo ukapita, ulipoingia mwaka 2011 mwezi wa kwanza ndipo nilipofanikiwa kubeba ujauzito wa Oscar.
Nilifurahi sana baada ya kuubeba ujauzito huo, niliamini huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuyaanza maisha mapya ya familia lakini ilikuwa ni tofauti kabisa na mawazo yangu.
Oscar alibadilika ghafla! baada ya kumpa taarifa hizo za ujazito, hakuwa Oscar yule niliyekuwa nikimfahamu, hakutaka kuamini kama nilikuwa nimebeba ujauzito wake, hilo lilizidi kumchanganya sana.
Nilishindwa kuelewa ni nini kilichokuwa kikiendelea, nilishangazwa na mabadiliko yake na hata nilipomuuliza nilishangaa akinigombeza na kunitolea maneno makali.
Nilihisi kuchanganyikiwa, sikutaka kuamini kama Oscar aliukataa ujauzito wake, hilo lilizidi kuniumiza sana, nilishindwa kuvumilia machozi yakaanza kunidondoka mfululizo.
Wakati nilipokuwa katika maumivu ya kukataliwa ujauzito ndipo hapohapo ambapo nilipokea maumivu mengine nisiyoyatarajia katika moyo wangu, Oscar aliamua kunieleza ukweli wa maisha yake.
Aliniambia alikuwa ni mume wa mtu na kipindi hicho mke wake ndiyo alikuwa akikaribia kurudi kutoka safarini.
Nilihisi kuchanganyikiwa baada ya kusikia maneno hayo, niliyakumbuka yale maneno niliyowahi kuambiwa na baadhi ya majirani lakini kutokana na kiburi changu sikutaka kuwasikiliza.
Mapenzi hatimaye yakaniingiza katika dunia ya maumivu na machozi, sikujua nilitakiwa kulia na nani kwani kama kuonywa nilionywa sana lakini sikutaka kusikia la mwadhini wala la mnadi swala.
“Kwahiyo unaamuaje?” nilimuuliza.
“Kuhusu nini?” aliniuliza.
“Huu ujauzito wako?”
“Mwajuma wewe ni chizi, mpumbavu, mshenzi, fala, hujielewi kabisa hivi unahisi ninaweza kuwa baba wa huo ujauzito wako? nenda katafute Baba halali lakini siyo mimi,” aliniambia Oscar maneno yaliyonifanya nitokwe na machozi. Nilishindwa kuzungumza, niliendelea kulia.
Kama ni makosa tayari nilikuwa nimeshayafanya. Kitendo cha kuishi na mwanaume bila ndoa, nikamuamini pasipokutegemea kama mwisho wa siku ningeweza kuvuna maumivu, hakika lilikuwa ni kosa kubwa mno nililolifanya.
Hatimaye Oscar aliweza kunifukuza, nikaanza kuishi maisha ya kutangatanga mitaani. Sikuwa na ndugu wala rafiki kusema labda ningeenda kumuomba hifadhi kwa muda, nilikuwa ni mimi na ujauzito wangu pekee.
Maisha yangu yalikuwa ni ya kutangatanga mitaani huku nikiomba msaada wa pesa na wakati mwingine nilikuwa nikienda kwa Mama Ntilie kuomba chakula, usiku ulipoingia nilikuwa nikilala nje, kiufupi hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu tangu nilipoweza kufukuzwa na Oscar.
Mwanzoni niliona ugumu kuishi maisha hayo lakini kadri siku zilivyokuwa zikizidi kusonga mbele, nilijikuta nikizoea na kuona ni maisha ambayo ni ya kawaida kuishi.
Siku moja nilikutana na msichana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Savela, aliponiona alihitaji kunisaidia. Nilipojitambulisha Savela alianza kunisifia, nikashangazwa na sifa zake yaani iliwezekana vipi msichana mwenzangu kama yeye akaanza kunisifia kama mwanaume?
Hilo lilinifanya nianze kuogopa, nilihisi Savela hakuwa mtu mwema kwangu, nilipokuwa nikimuangalia nikatamani anipe pesa kisha niondoke zangu.
Baada ya Savela kunihoji na kugundua mengi yaliyokuwa yamenitokea, alihitaji kunisaidia.
Nilisita kuchukua maamuzi ya haraka lakini baada ya kujifikiria maisha ambayo tayari nilikuwa nikiishi nilijikuta nikikubali tena bila kipingamizi chochote.
Alinichukua na kunipeleka mpaka nyumbani kwake alipokuwa akiishi maeneo ya Tegeta. Kwa muonekano wa nyumba yake jinsi ilivyokuwa ikionekana ilikuwa ni vigumu kuamini kwamba Savela ndiye ambaye alikuwa mmiliki wa nyumba hiyo, hakufanania kabisa.
"Hapa ni kwako?" nilijikuta nikiropoka na kumuuliza.
"Ndiyo hii ni nyumba yangu," alinijibu huku akionekana kuwa kawaida, hakujali lolote.
"Hongera ni nyumba nzuri sana," nilimwambia huku macho yangu yakiendelea kutazama sehemu za nyumba hiyo.
"Unaishi na nani?" nilimuuliza.
"Peke yangu," alinijibu.
Ilionekana kuwa ni nyumba kubwa iliyokuwa na vyumba vingi sana, kitendo cha Savela kuniambia kuwa aliishi peke yake kilinishangaza sana, sikutaka kuamini lakini huo ndiyo iliyokuwa ukweli.
Siku hiyo ikapita huku nikiwa nimeshapata bahati ya kufadhiliwa na Savela ambaye alionekana kuwa na moyo wa kipekee sana.
Hapa ngoja nikwambie kitu, nilikuwa mchafu sana, sikuwa na nguo zaidi ya niliyokuwa nimeivaa. Siku iliyofuata Savela aliamua kunipeleka kwenye duka la nguo maeneo ya Kinondoni, tulipofika huko alininunilia nguo, alinipeleka saluni ambapo huko nikazidi kupendezeshwa, ndani ya masaa kadhaa nilikuwa nimebadilika, sikuwa Mwajuma yule mchafu ambaye nilishindia nguo moja.
"Kwanini unayafanya yote haya?" nilimuuliza.
"Usijali Mwajuma nafanya haya kama masaada wangu kwako, najua umepitia magumu mangapi, sitaki kuona ukirudi kule wakati wewe bado ni msichana mrembo, unavutia, wasichana wenzako kama wewe mjini hawafi njaa, wanafanikiwa kiulaini," aliniambia maneno ambayo aliniacha nayo njia panda.
"Unamaanisha nini?"
"Usijali muda ukifika utajua namaanisha nini au wewe hupendi kuona ukiwa na maisha mazuri, ukamiliki nyumba ya kifahari, ukamiliki gari la gharama, ukawa mfanyabiashara mkubwa sana hapa mjini yaani kila mtu akawa anakuzungumzia wewe tu?"
"Napenda ila..."
"Basi kila kitu kinawezekana, mimi binafsi nimewahi kuishi kama yako, niliteseka mno, hakukuwa na mtu wa kunisaidia yaani kama sio mimi mwenyewe kujitambua sijui leo hii ningekuwa wapi?" alisema Savela kisha akaendelea kuzunguza.
"Umeiona ile nyumba yangu ya Tegeta nimeinunua juzi tu, nafanya biashara inayoniingizia pesa nyingi mno, sijasoma lakini nimeweza kufanya vitu vikubwa ambavyo wasomi wameshindwa kuvifanya," aliniambia Savela.
SEHEMU YA NANE
Kwa muda ambao Savela aliutumia kuzungumza na mimi tayari alikuwa ameipandikiza mbegu ya tamaa ya mafanikio ndani yangu, alijua kunishawishi, alijua kuzungumza yaani maneno yake yalitosha kunifanya nitamani kujua ni biashara gani hiyo ambayo alikuwa akiifanya.
SEHEMU YA TISA
Baada ya sekunde chache wasichana wawili wakaondoka na kubaki msichana mmoja, mazingira niliyoyaona yalitafsiri wazi kulikuwa kuna biashara ya uchangudoa iliyokuwa inafanyika, kuna muda yule msichana nilimuona akiwa anajigeuza sehemu za nyuma ya maumbile yake. Haikuchukua muda, msichana yule akaingia ndani ya gari kisha likawashwa na kuondoka.
"Mwajuma," aliniita Savela baada ya yule muhudumu kuondoka.
"Abee," nilimuitikia.
"Umemuona huyu muhudumu?"
"Ndiyo nimemuona kwani amefanya nini?"
"Kuna mtu amemuagiza aje kuniambia kuwa ananiita."
"Mtu gani?"
"Ni mwanaume."
"Mmh!"
"Subiri nikaongee naye," aliniambia kisha akainuka na kwenda kwenye meza iliyokuwa jirani kidogo na sisi.
Katika meza hiyo alikuwa amekaa mwanaume mmoja ambaye alionekana kuwa na mwili wa miraba minne, pembeni yake alikuwa amekaa msichana mmoja ambaye alionekana kuwa katika mavazi yaliyomuweka nusu uchi.
Savela alipofika katika meza hiyo nikamuona akikumbatiana na yule mwanaume, walionekana kama ni watu wanaofahamiana muda mrefu hivyo sikutaka kujaji sana, niliendelea kunywa soda yangu huku nikiwa sina wasiwasi wowote.
Bado niliendelea kuwashuhudia wasichana wakifanya biashara ya uchangudoa, biashara ilikuwa ikifanyika waziwazi wala hakukuwa na mtu aliyeonekana kuogopa au kushangaa, ilionekana kuwa ni biashara ya kawaida ambayo watu walizoea kuiona.
Nilibaki peke yangu katika meza hiyo mpaka pale ambapo Savela alirudi, aliniambia kuwa nilitakiwa kwenda kukaa naye meza moja na yule mwanaume aliyekuwa akizungumza naye, nilimkubalia kisha nikaenda kukaa naye katika meza ya mwanaume huyo, tulihamisha na vinywaji vyetu.
Yule msichana niliyemuona mwanzo akiwa amekaa na mwanaume huyo akainuka na kutupisha halafu nikamuona akimpa ishara fulani Savela ambayo nilishindwa kuielewa maana yake.
"Mwajuma huyu anaitwa Ibra, the big boss. Ibra huyu anaitwa Mwajuma ni msichana wangu na yeye ndiyo anainza hii kazi," alinitambulisha kwa mwanaume huyo ambaye nilishikana naye mikono.
"Okay..anaonekana kuwa mrembo sana aisee nahisi hata yale mambo yetu yatakuwa mazuri," alisema Ibra huku akitabasamu.
"Ndiyo hapo ni wewe tu sema kingine," alisema Savela kisha Ibra akanitazama, Savela akaniambia nisimame, nikafanya kama alivyoniambia.
Unajua huwa sipendi kujisifia sana lakini kwenye ukweli acha niwaambie, nilikuwa nina chura, nadhani ninaposema nilikuwa nina chura mmeshanielewa nini ninachokimaanisha, nilikuwa nina kila sifa zinazoweza kumteka mwanaume rijali.
Ibra aliponiona alizidi kupagawa, alikosa neno la kuzungumza kwa wakati huo, muda wote huo macho yake yalikuwa yakiangalia chura yangu.
"Mimi nilikwambia chombo si cha nchi hii," alisema Savela huku akitabasamu, aliimimina pombe kwenye glas kisha akanywa.
"Duh! Hiki chombo si mchezo ni balaa," alisema Ibra, wakati huo tayari nilirudi kukaa.
ITAENDELEA
SEHEMU YA KUMI
Mazungumzo yaliyokuwa yakizungumzwa mahali hapo yalikuwa ni ya kibiashara, Ibra muda wote alikuwa akanitazama.
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
Usiku wa siku hiyo nilihakikisha nimempagawisha Samir vya kutosha, ingawa kuna imani ipo kuwa wanaume ndiyo waliyozoeleka kuwa hatari zaidi wakati wa kufanya mapenzi na kuwaridhisha wanawake lakini kwangu ilikuwa ni kinyume chake, nilijua kufanya mapenzi na kumtoa jasho mwanaume, kukurukakara na purukushani zote za kitandani nilizijua.
Siku iliyofuata Samir alinilipa pesa kama tulivyokuwa tumekubaliana na huo ndiyo ulikuwa mwisho wa biashara yetu.
Japokuwa niliendelea kupata pesa lakini akili yangu ilikuwa ikifikiria kununua kiwanja kisha kuanza ujenzi wa nyumba yangu, nilikuwa nikifikiria pia kufungua biashara zangu mwenyewe.
"Fungua akaunti Facebook kisha Create page uanze kujitangaza, utapiga hela ndefu," alinishauri Savela nilipomuelezea mipango yangu.
"Hiyo imekaa vipi?" nilimuuliza.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"Ukifungua utakuwa ukipost picha na video za ngono halafu utakuwa ukitangaza biashara, lazima utapata wateja ila katika hizo picha utakazokuwa ukipost jaribu kuzikata kichwa usionekane," alinijibu kwa ufafanuzi kisha akaendelea kuzungumza.
"Biashara sasa hivi imebadilika, kuna wateja wengi sana mitandaoni, wapo baadhi ya wanaume wanaogopa kwenda Sinza kutafuta Malaya, wengine wanaogopa kuonekana, kwa kutumia njia hii ya mtandao ni lazima utawapata wateja wote hao tena wengine wapo nje ya nchi kama vile Kenya, Uganda na nchi nyingine," aliniambia.
"Na hao wateja wa nje ya nchi nitawafikiaje?"
"Wengine pesa ipo, wanakufuata au wanakutumia kila kitu, kazi yako ni kwenda kuwapa mapenzi tu."
Nilipoambiwa hayo nilishangaa, sikutaka kuamini kama mtandao wa Facebook ungeweza kunitengenezea kiasi kikubwa cha pesa kiasi hicho. Savela hakuishia hapo tu, aliendelea kuniambia jinsi biashara ya uchangudoa ilivyokuwa ikifanyika katika mitandao ya kijamii.
"Mmh ya kweli hayo?"
"Wewe endelea kuzubaa, wenzako tunazidi kupiga pesa hapa mjini, hatutumii nguvu nyingi halafu leo jioni kuna buzi mmoja naenda kukutana naye."
"Yupi huyo?"
"Ni wa Facebook, anaonekana ni mtu mwenye hela zake, leo lazima nikatanue nae," alinijibu Savela.
Nilihisi kuchanganyikiwa mno, nilipoambiwa biashara hiyo ilivyokuwa ikifanyika mitandaoni, nilitamani kuifanya.
Kwa kuwa nilimiliki simu ya kupangusa wala haikuwa kazi sana, nilichokifanya niliingia katika mtandao huo, nikajisajili, nikawa nina akaunti yangu, moyoni nilikuwa nina hamu kubwa sana ya kupata pesa na njia hiyo ndiyo niliiona kuwa rahisi ukitofautisha na ile ya kwenda kujiuza Sinza kwani kuna kipindi biashara ilikuwa ngumu kufanyika, muda mwingine wateja hawakupatikana kwa wakati.
Hakuna binadamu asiyeipenda pesa katika duniani hii, pesa ndiyo kila kitu, japo kuna baadhi ya watu hawaamini hilo, lakini huo ndiyo ukweli.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Sikia, mtu ukitaka kuvaa upendeze ni lazima pesa itatumika kununua nguo, ukitaka kula, kuishi maisha mazuri, pesa bado itahitajika na hii ndiyo sababu tunasema pesa ndiyo kila kitu.
Niliipenda pesa kuliko kitu chochote kile katika hii dunia, nilizaliwa katika familia yenye dhiki kubwa, wazazi wangu hawakuwa na pesa, niliishi maisha magumu mno nilipokuwa Mtwara, mpaka kufikia kipindi ambacho Bi Magreth mke wa Mzee Gidion anakuja kunichukua na kinileta mjini kwa lengo la kufanya kazi za ndani kiukweli sikutaka kuamini.
Kwa kuwa nilizaliwa katika familia iliyojaa dhiki hivyo nilitamani kuishi maisha mazuri. Kipindi ambacho Mzee Gidion alianza kunitongoza ilikuwa ni rahisi mimi kumkubalia kwasababu alitanguliza pesa, aliniahidi mambo mengi mazuri ambayo angeweza kunifanyia.
Naweza kusema tamaa ya pesa ndiyo iliyonifanya nikajikuta nikitembea na Daniel pamoja na Oscar.
Nilikuwa tayari nimeshafungua akaunti Facebook, nilikumbuka kufungua na ukurasa ambao niliutumia kupost picha zangu za utupu. Jina ambalo nilikuwa nikilitumia lilikuwa ni hili la Mwajuma Utamu.
Kazi niliyokuwa nimeibakiza mbele yangu ilikuwa ni mimi kujipiga picha za utupu kisha nikawa nazipost katika mtandao huo.
Mwanzoni wakati naanza kupost hakukuwa kuna like nyingi nilizozipata wala comment lakini kadri siku zilivyokuwa zikisonga ongezeko la watu waliyokuwa wafuatilaji wa ukurasa wangu huo waliongezekana tena kwa kiasi kikubwa sana.
Safari hii kila picha niliyokuwa nikiipost ilipata like nyingi na comment za kumwaga na hivyo wateja kuanza kujitokeza kwa wingi. Kwa kuwa niliweka namba yangu ya simu katika kila post, wateja hawakupata shida ya kunitafuta, walinipigia simu, tukaongea biashara na baada ya makubaliano biashara ya mapenzi ikafanyika.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu, nililala na wanaume wengi sana, ndani ya mwaka mzima nilikuwa nikiifanya biashara hiyo mpaka kufika mwaka 2013 nilikuwa tayari nimetengeneza kiasi kikubwa sana cha pesa.
Huwa sipendi kusimulia kila kitu nilichokuwa nikifanya wakati wa kufanya mapenzi kwasababu naamini maandishi haya yanasomwa na watu wa rika zote, ninachotaka kuwaandikia hapa ni mafunzo kwani biashara hii sio nzuri na sikushauri uifanye, nataka niwe mfano bora wa kukupa funzo fulani utakalojifunza baada ya kuisoma simulizi hii ya maisha yangu.
Kuna wasichana wengi sana hapa mjini ni matajiri, ni maarufu, wanapohojiwa na waandishi wa habari kusema siri ya mafanikio yao huwa wanadanganya, wanaficha kwa kusema kuwa wanafanya biashara inayowaingizia kiasi kikubwa cha pesa.
Sisemi haya kwa kuwakosoa wale wasichana wachapa kazi, wapo baadhi yao kweli wanafanya biashara, wameajiriwa katika makampuni makubwa na wanalipwa pesa ndefu tu.
Nilisafari mikoa mbalimbali ya nchi hii kama vile Mwanza, Arusha, Dodoma, Mbeya, Iringa na maeneo mbalimbali ya jiji la Daresalaam, nilikuwa nikiwafuata wanaume ambao nilienda kufanya nao mapenzi na ni kwasababu walikuwa na dau kubwa la pesa.
Siku ziliendelea kukatika, siku moja nilikutana na mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina la Martin Sepeku, huyu alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa sana hapa mjini.
Nilifanikiwa kulala naye, kwa kuwa nilifahamu alikuwa na pesa hivyo nilipanga kumpa mapenzi ambayo asingeweza kunisahau katika maisha yake, hilo nilifanikiwa tena kwa asilimia zote mia moja.
Taratibu akaanza kukolea, penzi langu likamlemvya. Katika kipindi hicho alikuwa bado hajaoa, alipofanikiwa kuuonja utamu wangu hakutaka kuukatisha, akaniambia kuwa alinipenda hivyo tukaingia katika mahusiano kwa miadi ya kunioa hapo baadae. Hilo halikuwa tatizo, nilimkubalia lakini moyoni mwangu sikumpenda isipokuwa nilizipenda pesa zake na huo ndiyo ulikuwa ukweli.
Sepeku akaanza kunionyesha mapenzi ya dhati, nilikuwa nina ndoto ya kumiliki nyumba, gari na vitu vingine vya thamani, vyote hivyo Sepeku aliahidi kunitimizia.
Baada ya kupita mwezi mmoja Sepeku alininunulia nyumba maeneo ya Msasani, ilikuwa ni nyumba ya kifahari na kama haitoshi pia akaninunulia gari pamoja na kunifungulia biashara mbalimbali.
Nilifurahi sana, ndoto yangu ilikuwa tayari imetimia lakini kama wasemavyo wahenga kuwa tabia siku zote hujenga mazoea, ndivyo ilivyokuwa kwangu, sikuacha biashara ya uchangudoa, niliendelea kuifanya lakini niliifanya kwa siri, Sepeku hakujua kilichokuwa kikiendelea katika maisha yangu.
Siku ziliendelea kukatika, baada ya miezi miwili kupita palianza kuzuka tetesi za jini mweusi ambaye alikuwa akiwachukua machangudoa na kwenda kuwaua.
Mauaji yalitokea na waliyokuwa wakiuwawa kikatili walikuwa ni machangudoa tu. Ni katika mauaji hayo Savela na yeye aliweza kuuliwa kikatili kisha mwili wake kutupwa katika ufukwe wa coco.
Kifo chake kiliniumiza mno, sio mimi tu niliyeumia zaidi bali hata machangudoa wengine waliumia pia.
Hali hiyo ilituogopesha sana, hatukujua muuaji huyo alikuwa ni nani na kwanini aliamua kufanya mauaji hayo. Kila changudoa alisema lake, tetesi ilizozagaa ni kuhusu Jini mweusi, yaani muuaji huyo aliitwa jini mweusi kwasababu waliyomuona walisema alikuwa akitembelea gari lenye rangi nyeusi.
Tetesi za jini mweusi zilitufanya tukaanza kuishi maisha ya hofu, kila changudoa akaanza kuwa makini na usalama wa maisha yake, gari lolote lenye rangi nyeusi lililoonekana likiingia na kupaki eneo hilo la Afrika sana tulipoliona tulikimbia, tuliamini ndiyo jini huyo mweusi aliyekuwa akiwaua machangudoa.
Hali ya sintofahamu ilitukumba, jeshi la polisi liliingilia kati, msako dhidi ya muuaji huyo ukaanza kufanyika lakini haikuishia hapo tu, pia walianza kuwakamata machangudoa na kuwafikisha mbele ya sheria.
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
"Nipe laki mbili tukalale baby wangu," nilimjibu.
SEHEMU YA KUMI NA TATU
Vyombo vya habari navyo havikuwa mbali, viliendelea kuripoti taarifa za muuaji huyo ambaye alisumbua sana na mpaka kufikia wakati huo hakukuwa na dalili zozote za kupatikana kwake.
Kipindi hicho ukurasa wangu ya Mwajuma Utamu ulikuwa umefikisha wafuatiliaji 500,000. Ulikuwa ni ukurasa ambao baadae niliutumia kwa kuwauza machangudoa wengine.
Suzie huyu alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu lakini pia alikuwa ni changudoa, alikuwa akiishi hostel. Nilifahamiana naye kipindi ambapo tetesi za jini mweusi zilivuma.
Suzie alipofahamu nimepata mwanaume tajiri ambaye alininunulia gari pamoja na nyumba ya kifahari maeneo ya Msasani, hakutaka kuamini, alionekana kunishangaa kupita kawaida.
Kwa jinsi alivyokuwa akiniangalia usoni, macho yake yalionyesha kuniuliza kwanini niliendelea kufanya biashara ya uchangudoa wakati nilipata mwanaume ambaye alikuwa na pesa na tayari alinifanyia mambo makubwa katika maisha yangu. Kama tatizo ni biashara alinifungulia tena zaidi ya moja.
“Kwanini usitulie tu na Martin, anaonekana kweli nakupenda?” aliniuliza Suzie.
“Hapana siwezi,” nilimjibu
“Kwanini au hujampenda?”
“Sijazoea kuwa na mwanaume mmoja katika maisha yangu, nisipofanya mapenzi na wanaume zaidi ya wawili najiona kama sijakamilika.”
“Jitahidi kwa Martin, anaonekana kuwa mtu mwema kwako.”
“Nitatulia lakini sio sasa, acha niendelee na uchangudoa wangu mpaka pale nitakaposema basi.”
“Sawa ila kuwa makini maana siku akigundua kuwa wewe ni changudoa nadhani huo ndiyo unaweza kuwa mwisho wa mahusiano yenu.”
“Hilo haliwezi kutokea na hata kama likitokea siogopi kitu kwanza nishamchuna sana,” nilimwambia.
Urafiki wangu na Suzie uliendelea kila siku, nilimshauri ajipige picha za utupu kisha nikamuweka katika ukurasa wangu, huko nilimtafutia wateja, nikamuunganisha nao, safari ya kupiga pesa mitandaoni ikaendelea.
Nilifanya mambo yote hayo lakini Martin Sepeku hakufahamu kilichokuwa kikiendelea, alikuwa ni mtu wa kusafiri mara kwa mara. Safari zake nyingi zilikuwa ni za nje ya nchi hivyo ilikuwa ni vigumu kugundua lolote.
“Nataka kukuoa Mwajuma uwe mke wangu kabisa,” aliniambia Martin siku moja kabla ya safari yake ya kwenda Dubai.
“Unafikiri itawezekana?” nilimuuliza.
“Kwanini isiwezekane kwani ugumu uko wapi?”
“Dini.”
“Dini sio tatizo mpenzi wangu ninachokitaka ni kufunga ndoa na wewe, nakupenda sana Mwajuma.”
“Nakupenda pia Martin lakini….”
“Nipo tayari kubadilisha dini kwasababu yako, nikirudi kutoka Dubai nataka nihalalishe mahusiano yetu au hupendi kuona siku nakuwa baba wa watoto wako na wewe unakuwa mama wa wanangu?”
“Napenda.”
“Basi nikubalie hili litimie kwanza.”
“Sawa litatimia,” nilimjibu.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kichwa kilianza kuniuma baada ya kumsikia Martin alihitaji kufunga ndoa na mimi kipindi atakaporudi kutoka safari yake ya Dubai. Kiukweli sikuwa nimejipanga katika hilo wala moyoni mwangu sikuwa nina mapenzi ya dhati na Martin.
Nilichokuwa nimekifuata kwake ni pesa pamoja na mali alizonimilikisha. Suala la kufunga ndoa nililiona kuwa gumu hasa kwa mtu kama Martin ambaye sikumpenda kutoka moyoni mwangu.
Nilipomueleza Suzie habari hizo alionekana kufurahi, aliniambia nisikubali nafasi hiyo ipotee, alienda mbali zaidi na kuniambia kama angekuwa ni yeye angekubali tena bila kipingamizi chochote.
“Ungekubali?” nilimuuliza.
“Ndiyo mimi ningekubali shoga yangu, embu angalia jinsi maisha yalivyokuwa magumu, angalia tunavyoteseka katika biashara hii, wakati mwingine tunakutana na wanaume wenye maumbile makubwa, kwasababu tunahitaji pesa tunakubali kufanya nao mapenzi, tunapata maumivu makali sana, hivi hii biashara tutaifanya mpaka lini?” aliniuliza Suzie kwa uchungu kisha akaendelea.
“Kama huyo mwanaume anakupenda na ana malengo na wewe naomba utulie naye, hii biashara ni bora ukaachana nayo tu,”aliniambia.
Maneno ya Suzie yalianza kuniingia, niliyatafakari na kuona kuwa yalikuwa na ukweli mtupu lakini tatizo lilikuja sehemu moja, sikumpenda Martin kutoka moyoni mwangu, kwake nilifuata pesa na maslahi mengine ambayo nilikuwa tayari nimeshayapata.
Nilipoona Suzie ananig’ang’aniza nikubali kuolewa na Martin ilibidi nilimueleze ukweli kuwa sikumpenda kama alivyokuwa akiamini, nilimpendea pesa zake na hiyo ndiyo ilikuwa tamaa yangu.
Suzie aliendelea kunishauri nikubali kuolewa na Martin kwasababu alikuwa na pesa na pia alionekana kuwa na malengo na mimi, hakutaka kuona nikiipoteza bahati hiyo. Kwake ulionekana kuwa kama wimbo wa taifa.
“Hata kama humpendi lakini angalia jinsi alivyojitoa kwako hivi ni mwanaume gani ambaye anaweza akakubali kufanya mambo yote hayo hata kama anakupenda?”
“Usiuzungumzie moyo wangu Suzie, nimeshakwambia kuwa simpendi Martin mbona hunielewi na sioni sababu ya kuolewa naye.”
“Mwajuma unajua unaichezea bahati, wasichana wengi wanaitafuta bahati hiyo wanaikosa halafu wewe unaipata lakini unaichezea.”
“Suzie hivi hakuna stori zingine za kuzungumza?”
“Utakuja kuijutia bahati hii unayoichezea.”
“Sidhani kama kuna siku nitakuja kuijutia, kwanza hilo haliwezi kutokea halafu nimekumbuka baadae ninatakiwa nikameet na Damian.”
“Who is Damian?” (Damian ndiyo nani?)
“Mpenzi wangu, mume wangu mtarajiwa,” nilimjibu.
Suzie alibaki akinishangaa baada ya kumwambia nilikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine aliyejulikana kwa jina la Damian.
Hii ilionyesha picha ya umalaya, yaani sikutulia na mwanaume mmoja, maisha yangu yalikuwa ni ya kudangadanga leo nilikuwa kwa mwanaume huyu kesho nilikuwa kwa mwanaume mwingine.
Huyu Damian nilikutana naye kwenye klabu moja iliyojulikana kwa jina la La Charz ambayo ipo Sinza Mori.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mahusiano yetu yalianza mara baada ya kunichukua usiku mmoja na kwenda kufanya naye mapenzi nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Beach.
Alikuwa ni mwanaume mwenye uwezo mkubwa wakati wa kufanya mapenzi, ingawa nilishawahi kujiapiza kuwa sintokuja kujihusisha na mahusiano na mwanaume aliyenichukua kwa lengo la kwenda kufanya mapenzi lakini kwa Damian ilikuwa tofauti na kiapo hicho, nilijikuta nikianzisha mahusiano naye ya kimapenzi bila kutarajia.
Baada ya kupita kipindi fulani penzi likawa tayari limeota mizizi, nilikuwa sisikii wala sioni kwa Damian, wakati huo nilikuwa tayari nipo katika mahusiano na Martin.
Hata hivyo sikuacha biashara ya uchangudoa mitandaoni, niliendelea nayo kama kawaida.
Nilipomwambia Suzie kuwa nilikuwa katika mahusiano na Damian alionekana kunishangaa sana, alihitaji kumfahamu mwanaume huyo zaidi na hata nilipomwambia maisha yake alimuona kuwa wa kawaida sana.
ITAENDELEA
SEHEMU YA KUMI NA NNE
Damian alikuwa ni muuza magari show room, japokuwa nilijitahidi kumpamba lakini bado alionekana kuwa wakawaida, hakumfikia Martin kwa utajiri aliyokuwa nao.
“Simpendi,” nilimwambia.
“Kwanini usingemwambia ukweli akajua kuliko hivyo unavyompotezea muda wake?”
“Suzie hivi upo tayari kweli kuacha fuko la hela likupite?”
“Hapana lakini.”
“Sasa ndiyo ujue nilikuwa sina jinsi, acha nitumie pesa zake, moyo wangu haupo kwake, kwasasa moyo wangu unaishi kwa mwanaume mwingine ambaye ni Damian,” nilimwambia Suzie pasipo kujua kuwa baadae ningeweza kuumia na kumwaga machozi kwasababu ya mapenzi.
Usiku wa siku hiyo nilienda kukutana na Damian nyumbani kwake Mbezi Beach, siku hiyo niliacha mambo yangu yote, nilijua nitautumia usiku mzima kuwa naye hivyo nilijipanga kwa mechi ya usiku huo.
Nilipofika nyumbani kwake alinikaribisha huku akinitolea tabasamu pana, nilijihisi kuwa na furaha mno kila nilipokuwa nikimtazama Damian, alikuwa ni mwanaume aliyejua kuiteka akili yangu kisawasawa.
Baada ya stori za muda mfupi Damian aliandaa chakula kwani kilikuwa tayari, tulikula kwa pamoja huku furaha ikionekana kututawala, tulipomaliza kula tuliendelea kupiga stori mpaka pale ulipofika muda ambapo tulikuwa chumbani, wote tulikuwa kama tulivyozaliwa, kilichoendelea wakati huo hakifai kusimuliwa hapa ila wewe fahamu kuwa tulifanya mapenzi usiku huo.
Tulipomaliza kufanya mapenzi Damian aliniambia twende tukaoge ili tuondoe uchovu uliyokuwa umetutawala, nilifanya kama alivyonitaka nifanye, tulipomaliza kuoga tulirudi kitandani kwa ajili ya kulala.
Muda wote huo Damian alionekana kuwa mwenye furaha, nilihisi labda kwa mapenzi niliyompa siku hiyo ndiyo yalimfanya kuwa katika wakati huo.
Kipindi ambapo nilikuwa nimejilaza kitandani, nilianza kuhisi kichwa kikiniuma, maumivu yaliendelea kuongezeka mpaka ukafikia wakati maumivu yakawa yametawala kichwa kizima.
Nilipomwambia Damian kuhusu maumivu hayo ya kichwa haraka akaenda kuniletea maji kwenye glass, aliniambia niyanywe kwani yangeweza kuniponya. Nikafanya kama alivyoniambia.
Maumivu bado yaliendelea kuongezeka, nikaanza kuhisi kizunguzungu wakati huo kichwa kiliendelea kunigonga. Nilishindwa kuyavumilia maumivu hayo mwisho nikaanza kupiga kelele, Damian akaoneka kupagawa. Ni hapo ambapo nilijikuta nikilala usingizi wa nusu kifo, sikujua ni kitu gani kiliendelea tena mahali hapo.
****
Nilipata fahamu na kujikuta nipo katika chumba kimoja kilichoonekana kuwa kama gofu, mazingira ya chumba hicho yalitisha mno, hakukuwa kuna harufu nzuri iliyotoka eneo hilo, ndani ya chumba hicho palitawala harufu ya kinyesi pamoja na ya mizoga ya binadamu iliyoonekana kuoza na kisha kubaki mifupa tu.
Mazingira niliyoyaona ndani ya chumba hicho yalinitisha mno, nikatamani kuinuka na kukimbia lakini sikuweza kufanya hivyo kwani nilikuwa nimefungwa kamba miguuni na mikononi lakini pia mdomoni nilikuwa nimezibwa kwa gundi ya karatasi.
Kila nilichokuwa nikitamani kukifanya kwa muda huo nilishindwa, mwisho ilibidi nitulie kwani hata pale nilipojaribu kupiga kelele, sauti yangu haikuweza kutoka kwasababu ya ile gundi niliyozibwa nayo.
Nilikumbuka mara ya mwisho nilikuwa kitandani na Damian, sikujua ni nini kilitokea mpaka kikasababisha kunileta ndani ya chumba hicho. Bado niliendelea kujiuliza maswali ambayo kiukweli yalikosa majibu, sikujua mpaka kufikia muda huo nilikuwa eneo hilo kwasababu gani.
Baada ya kupita dakika kadhaa mara mlango wa chumba hicho ukafunguliwa kisha akaingia mwanaume mmoja ambaye alivalia mavazi meusi pamoja na mask iliyonifanya nishindwe kuitambua sura yake.
Alipoingia moja kwa moja akaja kunitoa gundi mdomoni, nikatoa pumzi ndefu kisha nikaanza kukohoa. Mwanaume huyo hakuonekana kujali lolote, alionekana kuwepo mahali hapo kwa ajili ya kukamilisha kazi yake, alichoamua kukifanya aliingiza mkono wake upande wa nyuma ya suruali kisha akatoa bastola halafu akanielekezea usoni kuashiria kuwa alidhamiria kunipiga risasi kwa muda huo.
Niliamini huo ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha yangu, nilikuwa nikitetemeka, japokuwa sikujua nilifanya kosa gani mpaka kufikia hatua ya kutekwa lakini mwanaume huyo alioenakana kudhamiria kuniua.
“Nimekukosea nini?” nilimuuliza mwanaume huyo kwa kujiamini, swali langu likaonekana kuwa kituko, akaitoa bastola kwenye paji la uso wangu kisha akaanza kucheka kama mwendawazimu.
“Nipo hapa kwa ajili ya kukuuwa kama nilivyowaua malaya wenzako,” alinijibu mwanaume huyo.
“Kivipi na nimekukosea nini?” nilimuuliza.
Maswali yangu yalianza kuonekana kuwa kero kwa mwanaume huyo, alichokifanya ni kuitoa ile mask aliyokuwa ameivaa, ni hapo ambapo nikaiona sura yake, haikuwa ngeni machoni mwangu.
“Damian!” niliita kwa mshangao mkubwa.
“Yeah..” aliitika kisha akawa anaibusu bastola aliyokuwa ameishika.
Nilihisi kuchanganyikiwa baada ya kumuona Damian mbele ya macho yangu, kwa maana hiyo yeye ndiye aliyehusika kuniteka, sikutaka kuamini hata kidogo.
“Huu ni mpango wa kukuangamiza kama nilivyowaangamiza malaya wenzako,” aliniambia kisha akaikoki bastola yake tayari kwa kunimiminia risasi.
“Unataka kuniua?”
“Ndiyo tena sasa hivi.”
Majibu ya Damian pamoja na muonekanao aliyokuwa nao uliitosha kuelezea kuwa yeye ndiye alikuwa jini mweusi ambaye jeshi la polisi lilikuwa likimtafuta usiku na machana, aliua machangudoa wengi sana na siku hiyo alikuwa katika mpango wa kuniua na mimi pia.
Sikutaka kuamini kama nilinasa kama mtego huo na nilichokuwa nikikisubiri ni kupigwa risasi kisha uwe ndiyo mwisho wa maisha yangu. Kumbukumbu za Savela zilianza kunijia pamoja na kifo chake cha kikatili alichouwawa, ile mizoga iliyokuwa imezagaa ya binadamu ilitosha kuniambia kuwa muuaji alikuwa ni Damian. Nilimchukia sana, nilimuona kuwa binadamu mwenye roho ya kinyama.
“Sali sala zako za mwisho,” aliniambia Damian wakati huo alikuwa ameninyooshea bastola.
Kiukweli niliamini huo ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha yangu, kimoyomoyo nilianza kusali sala zangu za mwisho, nilifahamu hata iwe vipi ni lazima ningetoka ndani ya chumba hicho nikiwa maiti.
Machozi yalianza kunitoka, kila nilipokuwa nikimtazama Damian nilihisi kukiona kifo changu ambacho muda wowote kilikuwa kinakwenda kutokea.
“Kabla hujaniua tafadhali naomba nitubu dhambi zangu ili hata nikifa huko niendapo mbinguni niende sehemu salama,” nilimwambia huku machozi yakiendelea kunitoka.
Alichokuwa akikisubiri Damian ni mimi kutubu dhambi zangu kisha anifyatulie risasi kama alivyokuwa amedhamiria, nilifumba macho yangu kisha nikaanza kumuomba Mungu anisamehe madhambi yangu kwani muda mfupi ningekuwa katika safari ya kwenda mbinguni.
Paa… paa ...paa…
SEHEMU YA KUMI NA TANO
Nilichokisikia wakati nilipokuwa nimefumba macho yangu ni milio ya risasi, niliamini risasi hizo nilipigwa mimi, nilipoyafungua macho yangu kwa mara nyingine sikutaka kuamini kile nilichokuwa nikikishuhudia. Niliuona mwili wa Damian ukiwa chini huku ukitapatapa, damu zilikuwa zikimtoka kutokana na risasi alizokuwa amepigwa.
Ghafla! niliwaona polisi wakiwa ndani ya chumba hicho, sikutaka kuamini kile kilichokuwa kimetokea katika maisha yangu, yaani kama sio kutokea polisi ningeshakuwa maiti siku nyingi.
Polisi walinisaidia kunifungua kamba nilizokuwa nimefungwa nazo miguuni na mikononi, siku hiyo ndiyo ilikuwa mwanzo wa kuokoka na kifo nilichokuwa nimekikaribia.
Polisi walionekana kufanikiwa kazi yao kwa asilimia mia moja kwani muuaji huyo aliwasumbua mno, siku hiyo ndiyo walifanikiwa kumkamata na baada ya kumpiga risasi alifariki dunia hapohapo.
****
Baada ya kunisurika kifo na Damian au jini mweusi kama alivyokuwa akijulikana niliachana na biashara ya uchangudoa, sio mimi tu bali hata Suzie na yeye alichana na biashara hiyo.
Jambo la kushangaza baada ya Martin kurudi kutoka Dubai, Suzie aliitumia nafasi hiyo kumueleza kila kitu ambacho kilitokea katika maisha yangu.
Martin alinichukia baada ya kuambiwa hayo na kama haitoshi aliamua kuhamisha mapenzi kwa Suzie ambapo walifanikiwa kufunga ndoa na kubahatika kuzaa watoto mapacha, Gracious na Precious.
Niliumia sana baada ya tukio hilo kutokea hata hivyo sikuwa na wa kumlaumu, maisha yangu niliyachezea mwenyewe.
Baada ya kupita miezi mitatu niliamua kwenda kupima, majibu yalionyesha kuwa nilipata maambukizi ya virusi vya ukimwi hivyo nilitakiwa kuanza kutumia vidonge vya ARV kwa ajili ya kuongeza siku za kuishi.
Ni pigo kubwa katika maisha yangu, kiukweli najutia mambo mengi tena machafu niliyoyafanya katika maisha yangu, idadi ya wanaume niliyotembea nao inafika mia tatu.
Maisha ya mjini yalinishinda, niliuza kila kitu nilichoachiwa na Martin kama zawadi katika maisha yangu. Japokuwa ni miaka mingi sana imepita tangu nilipoondoka nyumbani kwetu Mtwara lakini niliamua kurudi.
Sikuwa ni Mwajuma yule wa zamani tena ambaye nilionekana kuwa mrembo wa sura mpaka umbo la kumvutia mwanaume yoyoye rijali, huyu wa sasa nilikuwa naishi na virusi vya ukimwi na muda wowote Mungu anaweza kunichukua kwani afya yangu imezidi kudhoofika.
FUNZO: Katika maisha wakati mwingine jifunze kutokana na makosa ya mtu mwingine, nimeamua kukusimulia kumbukumbu za maisha yangu ili na wewe ujifunze kutokana na makosa niliyoyafanya.
Naomba ukimaliza kuisoma kumbukumbu hii uyachukue yale yote mazuri kisha uyafanyie kazi na yale yote mabaya tafadhali naomba usiyachukue. Narudia tena katika maisha wakati mwingine jifunze kutokana na makosa aliyoyafanya mtu mwingine.
MWISHO.